Showing posts with label Old is Gold. Show all posts
Showing posts with label Old is Gold. Show all posts

Tuesday, August 7, 2012

INTERVIEW YA NANCY SUMARY: OLD IS GOLD....... HAPPY BIRTHDAY MDADA


Ikiwa leo ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Mrembo Nancy Sumary, tujikumbushe mahojiano aliyowahi kuyafanya mwaka 2005 ambapo alifanya vizuri sana kwenye maswala ya urembo. Twende pamoja hapo chini kufuatilia mahojiano hayo
 Lengo likiwa ni kuonyesha kuwa Nancy Sumary alijiamini kwa kiasi gani na mwenye matumaini makubwa wakati wa maandalizi yake kuelekea Miss World, na alipewa sapoti ya kiasi gani na kamati ya Miss Tanzania ili angalau aweze kufanya vizuri katika shindano hilo.

Baada ya mawasiliano ya hapa na pale na mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga ndipo nilipokutana na MissTanzania Nancy Sumari kwenye ofisi za kamati hiyo zilizopo jengo la Mavuno House, ghorofa ya nne na kufanya mahojiano naye kama ifuatavyo.
Mwandishi : Miss Tanzania Nancy Sumary hujambo dada?.

Nancy : Mimi sijambo kaka namshukuru Mungu.

Mwandishi : Tunaomba utupe historia yako kwa ufupi.

Nancy : Anatoa kicheko na kuonyesha tabasamu la kuvutia huku akianza kwa kusema “Mimi nimezaliwa miaka 19 iliyopita na nimepata elimu yangu nchini kenya, ambapo nilisoma huko mpaka kidato cha nne katika shule inayoitwa Maasai High School.”
Mwandishi : Kama unavyojua unakabiliwa na kazi ngumu ya kuwatoa kimasomaso Watanzania kwenye shindano la Miss World vipi maandalizi yako yamefikia wapi hivi sasa.?

Nancy : Kwa ujumla maandalizi sio mabaya yanaendelea vizuri na ninapata msaada mkubwa kutoka kamati ya Miss Tanzania nafikiri nitafanya vizuri tu.

Mwandishi : Unaweza kutupa ratiba yako ya kila siku jinsi unavyoipanga na kuifanyia kazi katika kujiandaa.?