Showing posts with label EVANS BUKUKU. Show all posts
Showing posts with label EVANS BUKUKU. Show all posts

Thursday, August 30, 2012

STAND UP COMEDY: EVANS BUKUKU ON 28/08/2012





 Mchekeshaji Maarufu Nchini kutoka Vuvuzela Entertainment,Evans Bukuku akikafanya vitu vyake usiku wa kuamkia leo katika kiota cha maraha cha Nyumbani Lounge,Namanga jiji Dar wakati wa Shoo yake ya kuvunja mbavu za watu (kuchekesha katika stand up comedy).
 Evans Bukuku akiendelea kuchana mbavu za watu kwa vituko vyake wakati wa Shoo yake ya kuvunja mbavu za watu (kuchekesha katika stand up comedy) iliyofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye kiota cha maraha cha Nyumbani Lounge,jijini Dar.
 Evans Bukuku akimuuliza mmoja wa wadau wake swali la kizushi kuhusiana na mambo ya kuchimba dawa safarini.
 Dogo Pepe wa Vuvuzela akionyesha umahiri wake wa kuvunja watu mbavu kwa kucheka wakati wa shoo yao iliyofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye kiota cha maraha cha Nyumbani Lounge,jijini Dar.
 MC wa Shoo hiyo alikuwa ni Taji Liundi nae haachi kuchekesha awapo stejini.
 Enika akiimba nyimbo za vichekesho.
Mmoja wa Wadau wakubwa wa Stand up Comedy za Evans Bukuku,aitwaye Ester Ulaya nae hakuwa nyuma kuotoa kituko chake wakati shoo hiyo ikiendelea.
 Kila aliefika ukumbini hapo hakuacha kucheka kwani vichekesho vilinoga ile mbaya.