Monday, September 10, 2012

JUMAMOSI YANGU ILIENDA HIVI

Huyo dada ni muhudumu, hayo ni maeneo ya Kibada, Kigamboni
Mida ya saa 4 asubuhi nilipita hapo nikajipatia supu kwa Buku tu (1000/-)
Chapati hiyo na chai alikula jirani yangu niliyemkuta hapo mezani
Tukafika eneo lenye VYUKU WA KIENYEJI...hahaha neno Vyuku limenikumbusha mahala
Hawa ni kuku wa Kienyeji hukooooooo Kisarawe II
Hawajachakachuliwa hata kidogo....
Na bata wa kienyeji pia wapo wa kutosha
Marafiki niliowapata siku hiyo....niliwafurahia sanaaaa, wana upendo wa hali ya juuu
Wa kienyeji wanajichunga wenyewe hasa wakitoka nje...hawa walikuwa wanapata kimvuli cha ndani watoke nje kula wadudu na nyasi....hapo sasa supu yake.......

Wakaniambia Ester jichagulie Kuku umpendae ukamfaidiii
Nikakamatiwa niliyechagua



Nikambeba huyooooooooooo hadi home........

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Hiyo supu hiyo umeniacha hoi nimeitamani kweli...nimekupata kuhusu vyuku kukukumbusha mahala:-)