Tuesday, July 3, 2012

KUTOKA KWA MASANJA MKANDAMIZAJI....NIMECHEKAA

Ilitokea hivi karibuni!

Kulikua na mabosi wawili wa kampuni moja ambao walikua wanapenda sana kutoka pamoja hasa siku za mapumziko. Walikua wanawatumia madereva wao kuwapeleka kila wanapoenda.

Kama ilivo kawaida kila bosi hujuana na dereva wake au boosi kumjua vilivyo dereva wake. Siku moja, jumapili, wakiwa wametoka na kuelekea maeneo ya ufukweni walianza kuzungumza na mazungumzo yakawa hivi:

Boss 1: aisee nakuambia sijawahi ona dereva mjinga kama huyu niliyenaye!

Boss 2: aaaaah we waongea nini……….huwezi amini huyo dereva niliyenaye yaani hamnazo kabisa.

Wakaendelea kubishana kila mmoja akisema dereva wake ni mjinga zaidi ndipo ikabidi wathibitishe kwa kila mmoja kuonyesha ujinga wa dereva wake.

Boss 1 akamuita dereva wake.

Boss 1: eeeeh chukua hii elfu 20 nenda kaninunulie FLAT TV inch 50 dukani!

Dereva: sawa boss, vp niilete huku au nipeleke nyumbani?

Boss 1: ukiweza kununua ilete hapa.

Dereva akaondoka, boss 1 akasema: waona alivo mjinga yaani hata hajui kua kwa shilingi elfu 20 huwezi kupata FLAT TV INCH 50.

Wakacheka, Boss 2 akasema sasa ngoja umuone dereva wangu alivyo mjinga.

Boss 2: hebu nenda nyumbani kaniangalie kama nipo!

Dereva: sawa bosi

Dereva akaondoka, Boss 2: waona alivyo mjinga, mimi nipo hapa alafu ataenda nyumbani kuniangalia kama nipo

Wakacheka na kusema kweli huyu mjinga.

Upande wa pili wale madereva wakakutana na kuanza kuongea.

Dereva 1: huwezi amini sijawahi fanya kazi na Boss mjinga kama huyu.

Dereva 2: bora wewe mi wangu ni punguani kabisa hata sijui kapata wapi ubosi.

Dereva 1: sasa sikia kaniita sahivi ananiambia niende nikamnunulie FLAT TV inch 50, wakati anajua fika kabisa kua leo ni jumapili na jioni hii hakuna duka lililowazi kama sio ujinga ni nini??

Wakacheka!
Dereva 2: hahaha aisee ila hata hivyo hafikii kwa upunguani wa bosi wangu, eti kaniita pale ananiambia niende nyumbani kwake nikamuangalie kama yupo, ilhali anasimu pale angeweza tu kupiga kwa mkewe nyumbani amuulize kama yupo au lah na sio kunisumbua mimi mpaka niende kwake naharibu mafuta tu...!!

Wakabaki wakicheka kila mmoja kuendelea na alichotumwa!

Je nani mjinga???? Mabosi au dereva??

No comments: