Tuesday, March 5, 2013

HESHIMA NI NINI?????????

 Dada akihudumia Mgahawani
 Akinawisha wateja wake mikono
Amepiga magoti hasa huku akiendelea kuwanawisha

Neno la msingi la Kiebrania linalotafsiriwa kuwa “heshima” linamaanisha kihalisi “uzito.” Mtu ambaye anaheshimiwa anaonwa kuwa mzito au wa maana sana. Mara nyingi, neno hilohilo la Kiebrania linatafsiriwa pia katika Maandiko kuwa “utukufu,” neno ambalo linaonyesha zaidi heshima ya juu ambayo mtu mwenye kuheshimiwa anaonyeshwa. (Mwa. 45:13) Neno la Kigiriki linalotafsiriwa kuwa “heshima” katika Biblia linamaanisha kustahi, kuthamini, kuona kuwa -enye thamani. (Luka 14:10) Ndiyo, watu ambao tunawaheshimu ni wenye thamani sana kwetu.

Kuwaheshimu wengine kunahusisha nini? Kunaanza na kuwastahi. Kwa kweli, maneno “heshima” na “staha” mara nyingi yanatumiwa pamoja kwa sababu yanahusiana sana. Kuonyesha heshima kunamaanisha kuonyesha staha kwa nje au waziwazi. Kwa maneno mengine, staha inahusiana hasa na jinsi tunavyomwona ndugu yetu lakini heshima inahusiana na jinsi tunavyomtendea ndugu yetu.

Je! Wewe unaelewaje neno HESHIMA?

4 comments:

Yasinta Ngonyani said...

HESHIMA---MAELEZO YAKE NI SAWA KABISA...ni alama ya kuthaminiwa, utu, adabu...ahsante kwa somo..

Interestedtips said...

kweli dada

Unknown said...

Asante Ubarikiwe na Bwana

Unknown said...

Nimepata kitu kizuri hapa