Sunday, September 16, 2012

BRIGITER ALFRED ANYAKUA TAJI LA REDD'S MISS KINONDONI 2012

  Mshindi wa shindano la Redds Miss Kinondoni Brigiter Alfred, akiwapungia mkono mashabiki walioshuhudia shindano hilo jijini Dar es Salaam jana, kulia ni mshindi wa pili Diana Hussein na mshindi wa tatu Irene David. Brigit pia anashikilia taji la Redds Miss Sinza 2012 huku Irene akishikilia taji la Miss Ubungo 2012. Pamoja na hayo Redd's Miss Kinondoni 2012 alijishindia taji la Miss Talent iliyokuwa umedhaminiwa na Perfect Lady Classic Saloon iliyopo Kinondoni jijini Dar na wamempa zawadi ya kupewa huduma kwa kipindi cha mwaka mzima
 ndani ya Saloon yao.
Akivalishwa taji lake la Redd's Miss Kinondoni 2012.
Mkurugenzi wa Perfect Lady Classic Saloon, Ester Kiama ambao ndiyo waliokuwa wamedhamini Redd's Miss Kinondoni Talent akitangaza zawadi alizompatia mrembo aliyeshinda, ambaye ni Brigiter Alfred (mrembo wa katikati).
Top 5 ya Redd's Miss Kinondoni 2012.
 Huyu ni Redd'd Miss Kinondoni 2012 aliyejinyakulia taji la kuwa Miss Mwananyamara Hospitali ambao kazi yake kubwa ni kuhamasisha kuchangia mfuko wa akina mama.

No comments: