Tuesday, September 18, 2012

DODOMA YETU ALONG RAILWAYBAADHI TU YA VIJIJI

 Station ya Dodoma Mjini.....train ilifika mida ya saa 2 asubuhi...wakashuka washukao...wakapanda wapandao....na tukashuka kuvuta pumzi na kuzunguka zunguka kidogo kabla safari kuendelea

 IDODOMYAAAAAAA
 Zao la Dodoma Wine.......tukauziwa tukabeba zawadi
Mabehewa ya Mizigo
 Vyumba vimepunguza mvuto, vitanda na mikanda yake imeishaaa......napenda kitanda cha juu na nilala hicho
 First Class ni ya Vitanda Viwili tuuuu....
 Juu na Chini ni Mnyororo jumla ya mabehewa 15 kama sikosei nilihesabu hivyo ukijumlisha na Engine/Kichwa yanakuwa 16

 Hiki kijiji kinaitwa Zuzu...sasa sielewi walikuwa na maana gani kukiita hivyo
Dodoma Inasifika kwa Ukame.....Check Ardhi Ilivyonuna

 Ubuyu na Ukwaju unapatikana kwa wingi Mkoa huu...ni mazao yanayostawi sana sehemu za Ukame...Hiki ni Kijiji Kingine
 Ndoo kama hii wanauza elfu mbili mia tano
 Kile paleeeeeeeeeee ni kisima cha maji cha kupump
 Asili yao Nyumba za Tembe
 Vikapu na Mifagio kwa wingi.............
Kofia za Kiasili kabisa zinauzwa....Hiki ni kijiji kingine tena baada ya Dododma Mjini
 Mtoto akifanya Biashara ya Mifagio akiwahi kwa style ya ki- Usain Bolt kupeleka kwa abiria kuwauzia 
Abiria wakiwahi Train iliposimama kwani kwenye vijiji kama hivi huwa inasimama kwa Dakika 2, zikizidi kunakuwa na shughuli isiyokwepeka........then inaendelea na safari
 Watoto wakifanya biashara ya ukwaju.......Mdau unaliongeleaje hili?
 Maskini huyu baba tulimuta kijiji kingine...inaonekana mzigo ulikuwa mzito...sasa kabla hajapanda na zile dakika 2 za Train kusimama ikaondoka kabla hajafanikiwa kupanda, ikamuacha duh
Babu akiwa busy akiuza Kofia

No comments: